DHNA YA SENTENSI: MTAZAMO WA KIISIMU
DHNA YA SENTENSI: MTAZAMO WA KIISIMU
Sentensi
Sentensi ni kipashio kikubwa kabisa cha kimuundo chenye maana kamili. (Massamba na wenzake, 2012:136). Nao Roberts N. B na Spancer A (2007:3) wanaeleza kwa kimombo kuwa “sentensi ni mpangilio au mfuatano wa maneno ambao huanza na herufi kubwa na kuishia kwa kituo kikubwa, ambapo kwa kawaida hutumika kuelezea au kufafanua hali ya mambo au vitu duniani.” (Tafsiri ni yangu)
Fasili hizi ni sahihi kabisa na kwa mwelekeo huo, tunaongezea kwa kusema kuwa sentensi ni kiwango cha juu kabisha katika viwango-madarajia ya tungo; ambacho, kwacho kinakuwa na maana iliyotimilika.
Sifa za sentensi
Sentensi zinazo sifa zake ambazo zinazisheheni ndani kwa ndani kama zikichunguzwa kwa undani kwa jicho la kisarufi zaidi. Baadhi ya sifa hizo, ni hizi zilizoorodheshwa:
i. Sentensi ni tungo ya kiwango cha juu kabisa katika viwango vya tungo.
ii. Sentensi zinajibainisha zaidi kimuundo. Hii ina maana ya kuwa sentensi hujistili na kupata uamilifu wake hasa ikitazamwa au kuchunguzwa katika sarufi miundo (sintaksia).
iii. Sentensi ni kipashio chenye maana iliyokamilika.
iv. Sentensi zina miundo yake mbalimbali.
v. Sentensi za Kiswahili zina miundo yake mahususi (taz. SAMIKISA, 2012:137-152).
vi. Sentensi ni utungo ambayo una sehemu kuu mbili, yaani mtenda na mtendwa (kiima na kiarifu au kikundi nomino na kikundi kitenzi/ kirai nomino na kirai kitenzi).
Hizi ni baadhi ya sifa bainifu za tungo sentensi ambazo kwa kiasi kila sentensi huwa nazo.
Aina za sentensi
Sentensi kama tungo, zinajibainisha kwa aina zake. Na aina hizi za sentensi zineainishwa katika mitazamo miwili tofauti ambayo ni mtazamo wa uainishaji sentensi kimuundo na mtazamo wa uainishaji sentensi kimaana.
Uainisha wa sentensi kimuundo
Uainishaji huure wa tungo sentensi huzingatia muundo (au umbo ) wa sentensi zaidi. Katika uainishaji huu tunapata aina nne (4) za sentensi, ambazo ni:
Sentensi sahili;
Sentensi ambatani;
Sentensi changamani.
Sentensi shurutia.
Kwa uanishaji wa kimuundo, sentensi zilizotajwa hapo juu ndizo aina za sentensi. Ikumbukwe kuwa hapa sentensi zimeainishwa kimuundo na si vinginevyo.
1. Sentensi sahili/huru
Habwe na Karanja wanasema kuwa hii ni sentensi ambayo ina kitenzi kikuu kimoja. Wakiwa na msisitizo kwamba sentensi ya/za aina hii si lazima zi/iwe rahisi kueleweka kimaana au zi/iwe fupi katika muundo wake. Ni sentensi yenye kueleza wazo moja tu ambalo hubebwa na kishazi kikuu hicho. Na Massamba na wenzie, wanafasili aina hii ya sentensi kwamba ni muundo wa tungo-sentensi unaohusisha kirai-nomino na kirai-kitenzi, na wenye maana kamili iliyokusudiwa. Kwa hiyo, sentensi sahili ni sentensi ambayo ina muundo wa kikundi-nomino na kikundi-tenzi yenye maana kamili iliyobebwa ndani ya wazo moja lililokusudiwa.
Mifano:
a) Baba ananipenda sana.
b) Kuku wangu ametotoa vifaranga vingi.
c) Anatembea.
d) Huyu ni mwalimu.
e) Marwa anasoma sana.n.k.
Mifano iliyobainishwa hapo juu ni sentensi sahili/sentensi huru, ambazo zina kikundi-nomino na kikundi-kitenzi na pia zimebeba maana na wazo moja lililokusudiwa. Sentensi sahili zina miundo yake. Na hii ifuatayo ni miundo ya sentensi sahili:
a) Muundo wa kirai-kitenzi.
- Nimekula.
- Anacheza.
- Wanalima.
Katika muundo huu, kirai-kitenzi kimesimama pekee kama sentensi sahili na kirai-kitenzi kimeundwa na kitenzi kimoja tu.
b) Muundo wa kirai- nomino na kirai-kitenzi.
- Felista anakuja.
- Vijana wanasoma.
- Wanakwaya wanaimba.
Kwenye sentensi hizi, inabainika wazi ya kwamba sentensi hizi zimeundwa na kirai-nomino kimoja na kirai-kitenzi kimoja.
c) Muundo wa virai-nomino na virai vitenzi vilivyokitwa katika kitenzi ‘kuwa’.
- Abasi ni kijana mzuri.
- Rugaenda yumo dukani.
- Abedi alikuwa kijana mwadilifu.
- Mwalimu atakuwa darasani kesho.
- Jane alikuwa na pesa.
- Kaka angekuwa wa kwanza.
Katika mifano ya sentensi iliyotolewa hapo juu, vitenzi vyake huchukuliwa kama miundo ya kitenzi kuwa katika wakati uliopo, na miundo hii yote inapowekwa katika nyakati tofauti nafasi yake huchukuliwa na kitenzi kuwa.
d) Muundo wa virai-nomino na virai-vitenzi vilivyoandamana na vijalizo.
- Dada yangu alinunua mayai matata usubuhi.
- Liliani anatafuta nguo yake kabatini.
- Mrembo mzuri alinyeshewa mvua nyingi jioni.
Katika muundo huu virai-nomino vina nomino na vivumishi mbalimbali na virai-vitenzi vimefuatwa na vijalizo ambavyo ni nomino, vielezi na vivumishi.
2. Sentensi ambatani
Sentensi ambatani ni tungo iliyo na tungo mbili zilizounganishwa na kiunganishi. Ni sentensi moja iliyounganishawa na vishazi huru viwili. (Taz. Misingi ya Sarufi na SAMIKISA).Aina hii ya sentensi hubeba visha viwili ambavyo huwa vinaendana kimaana.
Mifano:
a. Wanachuo wa Katoke ni wasikivu ilhali wanachuo wa Butimba ni wakorofi.
b. Anita anawabishia walimu lakini Roda anawasilikiza.
c. Mwalimu Mustafa ni rafiki wa mwalimu Lackson na mwalimu James ni rafiki wa mwalimu Jonia.
d. Wanachuo wa mwaka wa kwanza wanafagia viwanja huku wanachuo wa mwaka wa pili wanafyeka.
Ukichinguza mifano hii, utaona kuwa kila tungo inajumuisha sentensi mbili ambazo ni huru na zikiunganishwa na kiunganishai kimoja. Viunganishi katika sentensi hizi ni ilhali, na, lakini na huku. Sasa tuone mifano ya miundo ya sentensi ambatani:
a) Muundo wa vishazi sahili tu (sentensi sahili zilizounganishwa).
- Amepigwa sana lakini hajaumia kupita kiasi
- Tutangulie na wao watufuate.
- Siogopi wala sitishiki.
Hapa sentensi zilizotungwa ni sentensi ambatani ambazo kila sentensi imeundwa na sentensi sahili mbili zilizounganishwa na kiunganishi.
b) Muundo wa vishazi sahili na changamani (sentensi sahili na changamani).
- Wazazi waliokuwa hapa asubuhi wamerudi kwao lakini watoto wao hawakurudi.
- Chakula kizuri kimeiva wakati mpishi aliyekipika ameondoka.
- Wanafunzi wangu wameshindwa kufaulu mtihani lakini wale waliokuwa wamerudishwa kwao wamefaulu vizuri.
Katika sentensi hizi ni wazi kuwa sentensi sahili zimeambatana na sentensi changamani. Sentensi sahili ni vishazi huru na sentensi changamani ni vishazi changamani. Vishazi changamani vinadhihirishwa na urejeshi.
c) Muundo wa vishazi changamani tu (sentensi changamani zilizoungana)
- Ng’ombe aliyevimbiwa baada ya kula nyasi nyingi amechinjwa lakini mbuzi waliovimbiwa wamekufa.
- Vijana wale waliokuja hapa asubuhi wamerudi huku wasichana wao waliokuja nao hawakurudi.
Hakika ni wazi katika sentensi hizi kuwa zimeundwa na sentensi/vishazi changamani tu. Sentensi hizi zinazounda sentensi ambatani ni changamani kwani zimeundwa na vishazi virejeshi.
d) Muundo wa sentensi au vishazi visivyo na kiunganishi.
- Mwambie aondoke.
- Waite warudi.
- Wafuate uwaite.
Hizi nazo ni sentensi ambatani. Ni ambatani kwa sababu zimeundwa na sentensi sahili zenye virai-vitenzi vyenye kusimama kama sentensi sahili.
e) Muundo wa sentensi zilizounganishwa na koma/mkato (,).
- Mwalimu anafundisha, wanafunzi wanaandika.
- Wavulani ni watundu sana, wasichana ni wapole kupitiliza.
- Waandishi wa habari ni makasuku, wasanii ni watambaji.
Sentensi hizi ni ambatani zisizo na viunganishi vya maneno bali zimeunganishwa na alama ya koma au alama ya mkato.
3. Sentensi changamani
Sentensi changamani ni sentensi ambazo zina muundo wa kishazi tegemezi na kishazi huru. Ni sentensi ambazo zina mchanganyiko wa vishazi viwili tofauti. Wanasarufi wanasema ya kwamba sentensi ya namna hii angalau iwe na kishazi tegemezi kimoja na kisha huru kimoja. Kishazi tegemezi huhitaji kishazi huru ili kukamilika hasa kimaana. Tazama mifano yake hapa chini.
a. Kijana tuliyekutana naye mjini alikuwa mwalimu wetu.
b. Mtu alinunua kitabu kilichoandikwa na Mbaabu.
c. Aliporudi nyumbani alitukuta tumelala.
d. Kagero ambaye nilimfundisha amemaliza masomo yake.
e. Kwa kuwa hapendi nyama mpikie samaki n.k.
Sentensi hizi zimesheheni vishazi tegemezi na vishazi huru vinavyokamilisha vishazi tegemezi. Izingatiwe kuwa sio sheria kwa sentensi changamani kuwa na kishazi tegemezi kimoja tu; bali inaweza kuwa na zaidi ya kishazi-tegemezi kimoja. Ituatayo ni miundo ya sentensi changamani:
a) Muundo wa vishazi virejeshi.
Muundo huu ni ule ambao kipashio kikubwa kama kishazi hubebwa na kipashio kidogo kama kirai. Muundo huu ni ule ambao kirai-nomino hubeba kishazi kirejeshi (Massamba et al, 2012). Mfano:
- Kuku wetu tuliyemchinja kwenye sherehe nyama yake ilikuwa tamu sana.
- Maisha yaliyobora hayana vurugu nyingi.
- Binti aliyekuwa amekuja kututembelea jana anaitwa Stella.
- Nilipokuwa kwenye mafunzo kwa vitendo kule chuoni nilisingiziwa kuiba simu ya mwalimu wa shule ya msingi.
Sentensi hizi kwa sehemu kubwa zimeundwa na vishazi virejeshi, hasa katika sehemu ya virai-nomono.
b) Muundo wa vishazi vielezi.
Katika muundo huu, sehemu kubwa ya sentensi hujikita katika vishazi vielezi ambavyo hueleza hali ya vitenzi katika vishazi huru (Massamba et al, 2012). Kwa mfano;
- Alipokuwa mtoto alimpenda sana kaka yake.
- Akifaulu mtihani wake tutampongeza sana.
- Kwa sababu anapenda sana kuimba mpe gitaa.
- Tulitoka nyumbani asubuhi tukatembea kweli kweli.
Sentensi hizi zinaonesha kuwa zina vishazi vinavyoto maelezo zaidi kuhusu virai-vitenzi.
4. Sentensi shurutia
Hii ni aina ya sentensi ambazo zinakuwa zimeundwa na vishazi tegemezi tu. Huwa na utegemezi wa jambo moja kutegemea jambo lingine ili liweze kukamili. Huwa ni sentensi zente utegemezi wa kukamilishana ndani ya muundo wake. Katika sentensi hizi, kishazi tegemezi hutegemea kishazi kingine ili jambo linalolengwa likamilike. Mfano:
a) Angekuja leo tungeondoka leo.
b) Kama wangelijua wasingelitukosea.
c) Ningelikujua ningelikukong’ota.
d) Kama angaliona uzuri wake angalimuoa.
e) Japo asingeliniomba angalichukua.
Muundo wa sentensi shurutia huwa ni muundo wa vishazi tegemezi tu, vilivyoandamana.
Uainishaji wa sentensi kimaana
Uainishaji huu wa sentensi ulitiliwa maanani na wanasarufi mapokeo. Wao walizibainisha sentensi kimaana au kiuamilifu zaidi. Hawa ni waanzilishai wa sarufi ya lugha na wanajulikana kwa umashuhuri wao wa kuzichunguza tungo kwa kuangalia zaidi maana zake. Katika uanishaji huu, aina za sentensi zifuatazo zinabainika;
1) Sentensi taarifu
Hizi ni aina ya sentensi zenye kutoa taarifa fulani kuhusu kitu, mtu au jambo lolote. Mifano yake ni kama hii:
a. Ngedele amekula mahindi yangu.
b. Mjomba ameaga dunia leo.
c. Masuka ni mwnafunzi wa chuo cha ualimu Katoke.
d. Mwalimu ametuambia tusome kwa bidii ili tushinde mtihani.
e. Mboga za majani huongeza vitamini mwilini.
Sentensi hizi, uamilifu wake uko katika kujuza mambo fulani. Yaani zinatoa taarifa mbalimbali kama zinavyojidhuhirisha.
2) Sentensi ulizi (?).
Hizi ni sentensi zenye kudokeza jambo lenye kuhitaji majibu. Ni sentensi zenye kuuliza maswali yatarajiayo majibu. Huwa zina pengo katika sehemu yake ya taarifa (Habwe na Karanja, 2003:142). Ifuatayo ni mifano ya sentensi ulizi:
a. Nimekwambia ufanye nini?
b. Nyanya yako anaitwa nani?
c. Wewe umeruhusiwa na nani kugawa dafrati langu?
d. Kipi kikusikitishacho?
e. Kwa nini hukwenda kumsalimu mama yako?
Sentensi hiizi zinahitaji upande wa pili ili ziweze kupata kile kinachotarajiwa kujibiwa. Hivyo ni tungo zenye kuuliza na kutaka majibu.
3) Sentensi agizi.
Sentensi hizi hutoa maagizo yenye kuhitaji kutimizwa. Humwagiza msikilizaji kutenda kitendo fulani. Tazama mifano ifuatayo:
a. Leta hiyo kalamu!
b. Kamwite Pelanya aje hapa!
c. Fanya zoezi hili kabla ya saa nne na nusu!
d. Nenda nyumbani kwenu!
e. Zunguka uwanja mzima mara kumi!
Ukizichunguza hizi sentensi hizi, utagundua hali fulani ya uagizi ambayo msikilizaji anapaswa kutimiza.
4) Sentensi mshangao (!)
Hizi ni sentensi ambazo huonesha mshangao kwa tukio fulani, na huwa na alama ya mshangao (!). Katika wakati mwingine, sentensi hizi huitwa sentensi tashtiti zenye kuuliza maswali ambayo majibu yake hufahamika. Mfano wa sentensi hizi ni kama:
a) Aah, kumbe ni wewe!
b) Ati umeolewa?!
c) Ee, Mungu wangu!
d) Na wewe unajua kucheza?!
e) Wasalalee, umemwona amerudi akiwa njiti! n.k.
ALCHERAUS MUSHUMBWA, 2018
Sentensi ni kipashio kikubwa kabisa cha kimuundo chenye maana kamili. (Massamba na wenzake, 2012:136). Nao Roberts N. B na Spancer A (2007:3) wanaeleza kwa kimombo kuwa “sentensi ni mpangilio au mfuatano wa maneno ambao huanza na herufi kubwa na kuishia kwa kituo kikubwa, ambapo kwa kawaida hutumika kuelezea au kufafanua hali ya mambo au vitu duniani.” (Tafsiri ni yangu)
Fasili hizi ni sahihi kabisa na kwa mwelekeo huo, tunaongezea kwa kusema kuwa sentensi ni kiwango cha juu kabisha katika viwango-madarajia ya tungo; ambacho, kwacho kinakuwa na maana iliyotimilika.
Sifa za sentensi
Sentensi zinazo sifa zake ambazo zinazisheheni ndani kwa ndani kama zikichunguzwa kwa undani kwa jicho la kisarufi zaidi. Baadhi ya sifa hizo, ni hizi zilizoorodheshwa:
i. Sentensi ni tungo ya kiwango cha juu kabisa katika viwango vya tungo.
ii. Sentensi zinajibainisha zaidi kimuundo. Hii ina maana ya kuwa sentensi hujistili na kupata uamilifu wake hasa ikitazamwa au kuchunguzwa katika sarufi miundo (sintaksia).
iii. Sentensi ni kipashio chenye maana iliyokamilika.
iv. Sentensi zina miundo yake mbalimbali.
v. Sentensi za Kiswahili zina miundo yake mahususi (taz. SAMIKISA, 2012:137-152).
vi. Sentensi ni utungo ambayo una sehemu kuu mbili, yaani mtenda na mtendwa (kiima na kiarifu au kikundi nomino na kikundi kitenzi/ kirai nomino na kirai kitenzi).
Hizi ni baadhi ya sifa bainifu za tungo sentensi ambazo kwa kiasi kila sentensi huwa nazo.
Aina za sentensi
Sentensi kama tungo, zinajibainisha kwa aina zake. Na aina hizi za sentensi zineainishwa katika mitazamo miwili tofauti ambayo ni mtazamo wa uainishaji sentensi kimuundo na mtazamo wa uainishaji sentensi kimaana.
Uainisha wa sentensi kimuundo
Uainishaji huure wa tungo sentensi huzingatia muundo (au umbo ) wa sentensi zaidi. Katika uainishaji huu tunapata aina nne (4) za sentensi, ambazo ni:
Sentensi sahili;
Sentensi ambatani;
Sentensi changamani.
Sentensi shurutia.
Kwa uanishaji wa kimuundo, sentensi zilizotajwa hapo juu ndizo aina za sentensi. Ikumbukwe kuwa hapa sentensi zimeainishwa kimuundo na si vinginevyo.
1. Sentensi sahili/huru
Habwe na Karanja wanasema kuwa hii ni sentensi ambayo ina kitenzi kikuu kimoja. Wakiwa na msisitizo kwamba sentensi ya/za aina hii si lazima zi/iwe rahisi kueleweka kimaana au zi/iwe fupi katika muundo wake. Ni sentensi yenye kueleza wazo moja tu ambalo hubebwa na kishazi kikuu hicho. Na Massamba na wenzie, wanafasili aina hii ya sentensi kwamba ni muundo wa tungo-sentensi unaohusisha kirai-nomino na kirai-kitenzi, na wenye maana kamili iliyokusudiwa. Kwa hiyo, sentensi sahili ni sentensi ambayo ina muundo wa kikundi-nomino na kikundi-tenzi yenye maana kamili iliyobebwa ndani ya wazo moja lililokusudiwa.
Mifano:
a) Baba ananipenda sana.
b) Kuku wangu ametotoa vifaranga vingi.
c) Anatembea.
d) Huyu ni mwalimu.
e) Marwa anasoma sana.n.k.
Mifano iliyobainishwa hapo juu ni sentensi sahili/sentensi huru, ambazo zina kikundi-nomino na kikundi-kitenzi na pia zimebeba maana na wazo moja lililokusudiwa. Sentensi sahili zina miundo yake. Na hii ifuatayo ni miundo ya sentensi sahili:
a) Muundo wa kirai-kitenzi.
- Nimekula.
- Anacheza.
- Wanalima.
Katika muundo huu, kirai-kitenzi kimesimama pekee kama sentensi sahili na kirai-kitenzi kimeundwa na kitenzi kimoja tu.
b) Muundo wa kirai- nomino na kirai-kitenzi.
- Felista anakuja.
- Vijana wanasoma.
- Wanakwaya wanaimba.
Kwenye sentensi hizi, inabainika wazi ya kwamba sentensi hizi zimeundwa na kirai-nomino kimoja na kirai-kitenzi kimoja.
c) Muundo wa virai-nomino na virai vitenzi vilivyokitwa katika kitenzi ‘kuwa’.
- Abasi ni kijana mzuri.
- Rugaenda yumo dukani.
- Abedi alikuwa kijana mwadilifu.
- Mwalimu atakuwa darasani kesho.
- Jane alikuwa na pesa.
- Kaka angekuwa wa kwanza.
Katika mifano ya sentensi iliyotolewa hapo juu, vitenzi vyake huchukuliwa kama miundo ya kitenzi kuwa katika wakati uliopo, na miundo hii yote inapowekwa katika nyakati tofauti nafasi yake huchukuliwa na kitenzi kuwa.
d) Muundo wa virai-nomino na virai-vitenzi vilivyoandamana na vijalizo.
- Dada yangu alinunua mayai matata usubuhi.
- Liliani anatafuta nguo yake kabatini.
- Mrembo mzuri alinyeshewa mvua nyingi jioni.
Katika muundo huu virai-nomino vina nomino na vivumishi mbalimbali na virai-vitenzi vimefuatwa na vijalizo ambavyo ni nomino, vielezi na vivumishi.
2. Sentensi ambatani
Sentensi ambatani ni tungo iliyo na tungo mbili zilizounganishwa na kiunganishi. Ni sentensi moja iliyounganishawa na vishazi huru viwili. (Taz. Misingi ya Sarufi na SAMIKISA).Aina hii ya sentensi hubeba visha viwili ambavyo huwa vinaendana kimaana.
Mifano:
a. Wanachuo wa Katoke ni wasikivu ilhali wanachuo wa Butimba ni wakorofi.
b. Anita anawabishia walimu lakini Roda anawasilikiza.
c. Mwalimu Mustafa ni rafiki wa mwalimu Lackson na mwalimu James ni rafiki wa mwalimu Jonia.
d. Wanachuo wa mwaka wa kwanza wanafagia viwanja huku wanachuo wa mwaka wa pili wanafyeka.
Ukichinguza mifano hii, utaona kuwa kila tungo inajumuisha sentensi mbili ambazo ni huru na zikiunganishwa na kiunganishai kimoja. Viunganishi katika sentensi hizi ni ilhali, na, lakini na huku. Sasa tuone mifano ya miundo ya sentensi ambatani:
a) Muundo wa vishazi sahili tu (sentensi sahili zilizounganishwa).
- Amepigwa sana lakini hajaumia kupita kiasi
- Tutangulie na wao watufuate.
- Siogopi wala sitishiki.
Hapa sentensi zilizotungwa ni sentensi ambatani ambazo kila sentensi imeundwa na sentensi sahili mbili zilizounganishwa na kiunganishi.
b) Muundo wa vishazi sahili na changamani (sentensi sahili na changamani).
- Wazazi waliokuwa hapa asubuhi wamerudi kwao lakini watoto wao hawakurudi.
- Chakula kizuri kimeiva wakati mpishi aliyekipika ameondoka.
- Wanafunzi wangu wameshindwa kufaulu mtihani lakini wale waliokuwa wamerudishwa kwao wamefaulu vizuri.
Katika sentensi hizi ni wazi kuwa sentensi sahili zimeambatana na sentensi changamani. Sentensi sahili ni vishazi huru na sentensi changamani ni vishazi changamani. Vishazi changamani vinadhihirishwa na urejeshi.
c) Muundo wa vishazi changamani tu (sentensi changamani zilizoungana)
- Ng’ombe aliyevimbiwa baada ya kula nyasi nyingi amechinjwa lakini mbuzi waliovimbiwa wamekufa.
- Vijana wale waliokuja hapa asubuhi wamerudi huku wasichana wao waliokuja nao hawakurudi.
Hakika ni wazi katika sentensi hizi kuwa zimeundwa na sentensi/vishazi changamani tu. Sentensi hizi zinazounda sentensi ambatani ni changamani kwani zimeundwa na vishazi virejeshi.
d) Muundo wa sentensi au vishazi visivyo na kiunganishi.
- Mwambie aondoke.
- Waite warudi.
- Wafuate uwaite.
Hizi nazo ni sentensi ambatani. Ni ambatani kwa sababu zimeundwa na sentensi sahili zenye virai-vitenzi vyenye kusimama kama sentensi sahili.
e) Muundo wa sentensi zilizounganishwa na koma/mkato (,).
- Mwalimu anafundisha, wanafunzi wanaandika.
- Wavulani ni watundu sana, wasichana ni wapole kupitiliza.
- Waandishi wa habari ni makasuku, wasanii ni watambaji.
Sentensi hizi ni ambatani zisizo na viunganishi vya maneno bali zimeunganishwa na alama ya koma au alama ya mkato.
3. Sentensi changamani
Sentensi changamani ni sentensi ambazo zina muundo wa kishazi tegemezi na kishazi huru. Ni sentensi ambazo zina mchanganyiko wa vishazi viwili tofauti. Wanasarufi wanasema ya kwamba sentensi ya namna hii angalau iwe na kishazi tegemezi kimoja na kisha huru kimoja. Kishazi tegemezi huhitaji kishazi huru ili kukamilika hasa kimaana. Tazama mifano yake hapa chini.
a. Kijana tuliyekutana naye mjini alikuwa mwalimu wetu.
b. Mtu alinunua kitabu kilichoandikwa na Mbaabu.
c. Aliporudi nyumbani alitukuta tumelala.
d. Kagero ambaye nilimfundisha amemaliza masomo yake.
e. Kwa kuwa hapendi nyama mpikie samaki n.k.
Sentensi hizi zimesheheni vishazi tegemezi na vishazi huru vinavyokamilisha vishazi tegemezi. Izingatiwe kuwa sio sheria kwa sentensi changamani kuwa na kishazi tegemezi kimoja tu; bali inaweza kuwa na zaidi ya kishazi-tegemezi kimoja. Ituatayo ni miundo ya sentensi changamani:
a) Muundo wa vishazi virejeshi.
Muundo huu ni ule ambao kipashio kikubwa kama kishazi hubebwa na kipashio kidogo kama kirai. Muundo huu ni ule ambao kirai-nomino hubeba kishazi kirejeshi (Massamba et al, 2012). Mfano:
- Kuku wetu tuliyemchinja kwenye sherehe nyama yake ilikuwa tamu sana.
- Maisha yaliyobora hayana vurugu nyingi.
- Binti aliyekuwa amekuja kututembelea jana anaitwa Stella.
- Nilipokuwa kwenye mafunzo kwa vitendo kule chuoni nilisingiziwa kuiba simu ya mwalimu wa shule ya msingi.
Sentensi hizi kwa sehemu kubwa zimeundwa na vishazi virejeshi, hasa katika sehemu ya virai-nomono.
b) Muundo wa vishazi vielezi.
Katika muundo huu, sehemu kubwa ya sentensi hujikita katika vishazi vielezi ambavyo hueleza hali ya vitenzi katika vishazi huru (Massamba et al, 2012). Kwa mfano;
- Alipokuwa mtoto alimpenda sana kaka yake.
- Akifaulu mtihani wake tutampongeza sana.
- Kwa sababu anapenda sana kuimba mpe gitaa.
- Tulitoka nyumbani asubuhi tukatembea kweli kweli.
Sentensi hizi zinaonesha kuwa zina vishazi vinavyoto maelezo zaidi kuhusu virai-vitenzi.
4. Sentensi shurutia
Hii ni aina ya sentensi ambazo zinakuwa zimeundwa na vishazi tegemezi tu. Huwa na utegemezi wa jambo moja kutegemea jambo lingine ili liweze kukamili. Huwa ni sentensi zente utegemezi wa kukamilishana ndani ya muundo wake. Katika sentensi hizi, kishazi tegemezi hutegemea kishazi kingine ili jambo linalolengwa likamilike. Mfano:
a) Angekuja leo tungeondoka leo.
b) Kama wangelijua wasingelitukosea.
c) Ningelikujua ningelikukong’ota.
d) Kama angaliona uzuri wake angalimuoa.
e) Japo asingeliniomba angalichukua.
Muundo wa sentensi shurutia huwa ni muundo wa vishazi tegemezi tu, vilivyoandamana.
Uainishaji wa sentensi kimaana
Uainishaji huu wa sentensi ulitiliwa maanani na wanasarufi mapokeo. Wao walizibainisha sentensi kimaana au kiuamilifu zaidi. Hawa ni waanzilishai wa sarufi ya lugha na wanajulikana kwa umashuhuri wao wa kuzichunguza tungo kwa kuangalia zaidi maana zake. Katika uanishaji huu, aina za sentensi zifuatazo zinabainika;
1) Sentensi taarifu
Hizi ni aina ya sentensi zenye kutoa taarifa fulani kuhusu kitu, mtu au jambo lolote. Mifano yake ni kama hii:
a. Ngedele amekula mahindi yangu.
b. Mjomba ameaga dunia leo.
c. Masuka ni mwnafunzi wa chuo cha ualimu Katoke.
d. Mwalimu ametuambia tusome kwa bidii ili tushinde mtihani.
e. Mboga za majani huongeza vitamini mwilini.
Sentensi hizi, uamilifu wake uko katika kujuza mambo fulani. Yaani zinatoa taarifa mbalimbali kama zinavyojidhuhirisha.
2) Sentensi ulizi (?).
Hizi ni sentensi zenye kudokeza jambo lenye kuhitaji majibu. Ni sentensi zenye kuuliza maswali yatarajiayo majibu. Huwa zina pengo katika sehemu yake ya taarifa (Habwe na Karanja, 2003:142). Ifuatayo ni mifano ya sentensi ulizi:
a. Nimekwambia ufanye nini?
b. Nyanya yako anaitwa nani?
c. Wewe umeruhusiwa na nani kugawa dafrati langu?
d. Kipi kikusikitishacho?
e. Kwa nini hukwenda kumsalimu mama yako?
Sentensi hiizi zinahitaji upande wa pili ili ziweze kupata kile kinachotarajiwa kujibiwa. Hivyo ni tungo zenye kuuliza na kutaka majibu.
3) Sentensi agizi.
Sentensi hizi hutoa maagizo yenye kuhitaji kutimizwa. Humwagiza msikilizaji kutenda kitendo fulani. Tazama mifano ifuatayo:
a. Leta hiyo kalamu!
b. Kamwite Pelanya aje hapa!
c. Fanya zoezi hili kabla ya saa nne na nusu!
d. Nenda nyumbani kwenu!
e. Zunguka uwanja mzima mara kumi!
Ukizichunguza hizi sentensi hizi, utagundua hali fulani ya uagizi ambayo msikilizaji anapaswa kutimiza.
4) Sentensi mshangao (!)
Hizi ni sentensi ambazo huonesha mshangao kwa tukio fulani, na huwa na alama ya mshangao (!). Katika wakati mwingine, sentensi hizi huitwa sentensi tashtiti zenye kuuliza maswali ambayo majibu yake hufahamika. Mfano wa sentensi hizi ni kama:
a) Aah, kumbe ni wewe!
b) Ati umeolewa?!
c) Ee, Mungu wangu!
d) Na wewe unajua kucheza?!
e) Wasalalee, umemwona amerudi akiwa njiti! n.k.
ALCHERAUS MUSHUMBWA, 2018
Safi sana!
JibuFutaSentensi ni tungo lakni si kila tungo ni sentensi
JibuFutaMiumdo ya mine ya kiarifu
JibuFutaiko vizuri
JibuFutaRobert N.B na spancer wameandika kitabu gani kinachoelezea sentensi?
JibuFuta